BENDI ya Muziki wa dansi hapa nchini Mashujaa, inatarajia
kuwatambulisha wapya sita katika hafla itakayofanyika kesho katika Ukumbi wa
Zhonghua Garden Morocco Jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar leo, Meneja wa bendi
hiyo Martine Sospter alisema, wapya hao kutoka Kongo wanne ni wanenguaji na
wawili ni waimbaji ambao watasaidiana kazi ili kuimalisha bendi hiyo.
Sospter alisema, mbali na utambulisho huo, watatumia siku
hiyo kuwashukuru Watanzania kwa kuwateua hadi kuibuka bendi bora ya mwaka
katika kinyang’anyiro cha Kill Music Award 2013 kilichofanyika hivi karibuni.
“Sisi tunamshukuru mungu kwa kutufanya kuwepo imara mpaka
sasa, na hatutawaangusha mashabiki wetu kwani tunaukubali sana mchango wao wa
hali na mali na ndio maana tunawaomba wajitokeze kwa wingi Jumamosi ili
wajionee mambo mapya ikiwemo kuwatambulisha wasanii wapya na
wanenguaji,”alisema Sospter.
Aliongeza kuwa siku hiyo Msanii wa kizazi kipya Dully Sykes
atawasindikiza katika hafla hiyo.
Nae Mratibu wa bendi hiyo, Kingdodoo Bouche aliwataja wapya
hao kuwa ni, Gracia Mesu a.k.a John Boko, Bosawa Fany ‘Juma Kaseja’, Jolie
Kindu ‘Mrisho Ngasa’ na Patricia Nzomba ‘Mbwana Samata’ huku waimbaji akiwa ni
Jimmy Adoli na Eddy Mboyo.
Aliongeza kuwa kwa kuwa bendi yao ni imara na ni ya utaifa
ndo sababu ya wanenguaji hao kutumia majina ya wachezaji wa timu ya Taifa
‘Taifa Stars’.
No comments:
Post a Comment