HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, June 27, 2013

Mkazi wa Majengo Moshi anusurika katika ajali

Na Dixon Busagaga wa globu ya jami Moshi.

Mkazi wa majengo mjini Moshi aliyefahamika kwa jina la Frank Ngowi jana usiku amaenusurika kifo baada ya kugongwa na gari aina ya Hiace (daladala) lenye namba za usajili T352 AFM ikifanya safari zake kati ya Kiboriloni na katikati ya mji wa Moshi .

Ajali hiyo imetokea jana majira ya saa 3 usiku eneo la majengo polisi jirani kabisa na zahanati ya Kishamba.

Kwa mujibu wa mashuhuda wa ajali hiyo walisema kuwa dereva wa daladala hiyo ambaye jina lake halikuweza kufahamika mara moja alionekana amelewakupita kiasi.

Mashuhuda walidai dereva huyo baada ya kugundua amesababisha ajali alikimbia na kuelekea maeneo ya majengo sekondari ambapo waendesha bodaboda walimkimbiza na kufanikiwa kumkamata na kumrudisha mpaka kwenye eneo la ajali.

Askari polisi walifanikiwa kufika eneo la tukio na kumchukua dereva wa gari hilo pamoja na majeruhi kwa ajili ya hatua za awali.
Huu ndio usafiri aliokuwa akiutumia Bw Ngowi.
Baada ya dereva wa Hiece kufanikiwa kukimbia vijana walimkimbiza na kumshika na hapa walikuwa katika harakati za kumrudisha kwenye eneo la ajali.
Majeruhi wa ajali Frank Ngowi aliyegongwa na daladala wakati akiendesha baiskeli akionesha majeraha baada ya kupata ajali.
Hii ndio daladala iliyosababisha ajali na kufanikiwa kukimbia hata jitihada zilifanyika na kufanikiwa kukamatwa na kurudishwa katika eneo la ajali.
Jeshi la polisi lilifanikiwa kufika eneo la tukio.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad