Mstahiki Meya Jerry Silaa akisalimiana Mke wa Makamu wa Rais Mama Asha Bilal walipokutana kwenye Banda la Mfuko wa Fursa sawa kwa wote (EOTF) kwenye viwanja vya maonyesho ya Kimataifa ya Biashara jijini Dar.
Mwenyekiti wa Mfuko wa Fursa Sawa kwa Wote (EOTF) Mama Anna Mkapa akiagana na Mstahiki Meya Jerry Silaa mara baada ya kutembelea Banda la (EOTF) linalotoa fursa kwa wajasiriamali nchini Tanzania kuonyesha bidhaa zao katika maonyesho hayo kila mwaka.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Home Shopping Centre (HSC) Fahad Said Mohamed (kushoto)
akimkaribisha Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Silaa kwenye
Banda la HSC kwenye maonyesho ya 37 kimataifa ya Biashara yanayoendelea
katika uwanja wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam.
Mtsahiki
Meya Jerry Silaa akipewa maelezo ya jinsi Mfuko wa Fursa sawa kwa wote
unavyopambana na kutokomeza Ugonjwa wa Saratani ya Matiti kwa wakina
mama nchini. Kushoto ni Mwenyekiti wa Mfuko wa Fursa Sawa kwa Wote
(EOTF) Mama Anna Mkapa.
Mstahiki Meya Jerry Silaa akipata maelezo jinsi ya kutumia Kizimamoto Fanisi cha kurusha (Fire Extinguisher) ambacho ni rahisi kutumia na hakihitaji matengenezo na hudumu kwa miaka mitano pia Kifaa hicho ni rafiki wa mazingira na mvumbuzi bora kwa uokoaji wa dharura wakati alipotembelea Banda la GreenBat Fire Solutions katika maonyesho ya Sabasaba yanayoendelea.
Mstahiki Meya Jerry Silaa akisaini kitabu cha wageni katika banda la Arusha International Conference Centre (AICC) wanaoshughulika kutoa huduma za kumbi za Kimataifa za mikutano na Utalii jijini Arusha.
Mstahiki Meya Jerry Silaa akingalia jinsi mtoto Range Jackson ( wa pili kushoto) mwenye ulemavu wa Ubongo akionyesha ramani ya Tanzania na Sehemu ya mipaka yake iliyotumika kumfundishia kujua kusoma na kuandika na ufundi stadi kupitia kituo cha VETA. Kulia ni Mkufunzi wa kuchomea (Welding Instructor) na Mwalimu wa watu wenye mahitaji maalum Bw. Kintu Kilanga na Wa tatu kulia ni Baba mzazi wa kijana huyo Bw.Jackson Range.(Picha na Zainul Mzige).
No comments:
Post a Comment