HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, July 1, 2013

RAIS BARACK OBAMA AWASILI NCHINI MCHANA HUU

 Rais Barack Obama wa nchini Marekani na Mkewe Michelle Obama wakiwa sambamba na watoto zao,wakiwasili chana huu kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere,jijini Dar es Salaam mchana huu kwa ziara ya siku mbili hapa nchini.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimkaribisha Rais Barrack Obama wa Marekani muda mfupi baada ya kuwasili katika Uwanja wa ndege wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam mchana wa leo. Kulia ni Mke wa Rais Mama Salma Kikwete.
Rais Dkt.Jakaya Kikwete akiwa na mgeni wake Rais Barrack Obama wa Marekani muda mfupi baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam leo mchana.nyuma ya Rais na mgeni wake ni Mke wa Rais Mama Salma Kikwete na mke wa Rais wa Marekani Mama Michelle Obama.
Rais Barrack Obama akikagua gwaride la heshima lililoandaliwa na jeshi la Wananchi wa Tanzania(JWTZ).
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimtambulisha kwa Rais Barrack Obama wa Marekani Rais wa Zanzibar Dr.Ali Mohamed Shein muda mfupi baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam leo mchana.Huku Mke wa Rais Mama Salma Kikwete na Mke wa Rais wa Marekani Michelle Obama Wakiangalia.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimtambulisha kwa Rais Barrack Obama wa Marekani makamu wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Iddi muda mfupi baada ya Rais huyo wa Marekani kuwasili nchini kwa Ziara ya kikazi ya siku mbili.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimtambulisha kwa Rais Barrack Obama wa Marekani makamu wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Iddi muda mfupi baada ya Rais huyo wa Marekani kuwasili nchini kwa Ziara ya kikazi ya siku mbili.
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Jenerali Davis Mwamunyange akisalimiana na Rais Barrack Obama katika uwanja wa ndege wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam leo.
RaisDkt.Jakaya Mrisho Kikwete na mkewe Mama Salma Kikwete wakiwaongoza wageni wao Rais Barrack Obama wa Marekani na mkewe Michelle kuangalia ngoma mbalimbali za utamaduni muda mfupi baada ya kuwasili katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere kwa ziara ya siku mbili nchini.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete na mgeni wake Rais Barrack Obama wa Marekani wakifurahia na kufuata mapigo ya ngoma za utamaduni katika uwanja wa Ndege wa Mwalimu jijini Dar es Salaam leo mchana wakati wa mapokezi ya kiongozi huyo wa Marekani na ujumbe wake.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho kikwete akiwatambulisha baadhi ya viongozi waandamizi wa serikali kwa Rais Barrack Obama na mkewe katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam leo.Picha na Freddy Maro,Ikulu.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad